Thu, 16 Nov 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa klabu ya Wanawake ya Chelsea Emma Hayes ameteuliwa kuwa kocha mkuu wa timu ya Taifa ya Wanawake ya Marekani (USWNT) ambapo anatarajia kuwa kocha wa kike anayelipwa mshahara mrefu zaidi katika medani ya soka Duniani.
Hayes ambaye anatarajia kutia kibindoni mshahara wa pauni milioni 1.28 kwa mwaka, atakuwa akilipwa mara tatu ya mshahara wa kocha wa timu ya Taifa ya Wanawake ya England, Sarina Wiegman.
Hayes (47) raia wa England atajiunga na USWNT mwishoni mwa msimu wa 2023/24.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live