Fri, 13 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa zamani wa Azam FC, Vivier Bahati anatarajia kusaini mkataba muda wowote ndani ya timu ya Elaga Top Junior ya mkoani Makamba nchini Burundi baada ya kuachana na timu ya Bumamuru FC.
Vivier Bahati ambaye alikuwa ni kocha mkuu wa Bumamuru FC alikataa kuwa kocha msaidizi wa klabu hiyo baada ya kuletwa kocha mpya Joslin Bipfubusa ambaye wiki kadhaa alifukuzwa ndani ya Polisi Tanzania.
Mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Burundi umemalizika timu ya Bumamuru FC ikiwa kileleni mwa ligi na alama 32.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live