Thu, 25 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha wa timu za vijana za Azam FC, Mohamed Badru amemzungumzia Maxi Nzengeli kama silaha ambayo itakuwa ikiangamiza kimyakimya huku akiweka wazi kuwa nyota huyo amekuwa akimvutia sana.
Maxi amekuwa na kiwango bora sana msimu uliopita aliposajiliwa na na Klabu ya Yanga akitokea Maniema FC ya Congo DR.
“Binafsi ni kati ya wachezaji wa kigeni ambao navutiwa nao, ni mchezaji wa kitimu zaidi, unaweza kumuona kila eneo kwa sababu anauwezo wa kufanya hivyo, hakuna mchezaji wa namna hiyo ambaye anaweza kukaa benchi, anasifa za kipekee,” amesema kocha huyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: