Sat, 9 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada kulazimishwa sare ya bila kufungana na Timu ya Tanzania "Taifa Stars" Septemba 7 mchezo wa kuwania kufuzu kwa Mataifa ya Afrika AFCON.
Kocha wa Algeria, Djamel Belmadi ameonekana kutofurahishwa na uamuzi wa Chama cha soka nchini humo kupeleka mechi Annaba akidai ni uwanja ambao hauna ubora akitaja umeathiri ufanisi wa timu yake.
“Uwanja hauko tayari kuandaa mechi ya timu ya taifa, hivyo tunatakiwa kutafuta suluhisho lingine. Uwanja haupo kama ulivyokuwa mwezi Juni. haupo katika ubora ambao tunautaka kwa mechi ya kimataifa,” alisema Belmadi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live