Thu, 28 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha mkuu wa Al Ahly Marcel Koller ameahidi kuimaliza mechi yao dhidi ya Simba Benjamin Mkapa na hajali kuhusu rekodi ya michezo ya nyuma baina yao.
“Tumejiandaa vyema kuonesha kiwango bora kesho na tunakwenda kushinda kwa kuwa hatujaja kuangalia historia yetu na yao bali kucheza mpira”.
“Hatutacheza kwa ajili ya kusubiri kuumaliza mchezo nyumbani , tutacheza kwa umakini kwa nia ya kuumaliza Mchezo hapa hapa ugenini “
“Nimecheza nao (Simba) mechi (2) na zote tumetoa sare, niliwaona na naweza kusema kuwa wapo kwenye level kama yetu siyo wadogo kwa hiyo hatutawadharau”
Chanzo: www.tanzaniaweb.live