Viongozi wa bodi ya Ligi kuu nchini Afrika Kusini wametoa lawama zao kwa shirikisho la soka nchini Afrika Kusini kuhusu kiwango cha pesa anacholipwa kocha mkuu wa timu ya Taifa Hugo Broos kuwa ni kikubwa mno tofauti na kazi anayofanya.
Broos analipwa R750,000 sawa na USD 50,000 ambayo kwa pesa ya kitanzania Million 127 kiasi ambacho ni kikubwa tofauti na kile walichokuwa wanapokea makocha waliomtangulia Stuart Baxter na Pitso Mosimane waliokuwa wanapokea Million sita [R50,000].
Hata hivyo shirikisho la soka nchini Afrika Kusini limemkingia kifua kocha huyo ambaye ni mshindi wa fainali za mataifa ya Afrika mara moja.