Wed, 20 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Manchester United Christian Eriksen amefichua kuwa hana furaha klabuni hapo kutokana na kukaa benchi huku akitaka kupata muda zaidi wa kucheza.
Fabrizio Romano anaripoti kuwa Eriksen (32) raia wa Denmark amedai kuwa anahitaji muda wa kucheza zaidi tofauti na anaoupata kwa sasa.
Aidha Eriksen amebainisha kuwa tayari amezungumzia hilo na kocha Eric Ten Hag lakini kocha huyo amemuweka wazi kuwa kuna ushindani wa nafasi huku kiwango cha kinda Kobbie Mainoo kikitajwa kuwa chanzo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live