Wed, 20 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Baada ya kuwavuruga Liverpool kwenye robo fainali ya kombe la FA, kinda wa Manchester United, Kobbie Mainoo amejumuishwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa England.
Mainoo mwenye umri wa miaka 18 atakuwa sehemu ya kikosi cha England ambacho kitacheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Brazil Machi 23, 2024 na Ubelgiji Machi 26, 2024.
Mainoo ambaye wazazi wake ni Waghana alikuwa mmoja wa wachezaji walioonesha uwezo mkubwa katika ushindi wa 4-3 wa Manchester United dhidi ya Liverpool katika robo fainali ya kombe la FA
Chanzo: www.tanzaniaweb.live