Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amekutwa dalili za maambukizi ya virusi vya Covid-19 na atakosa mechi ya Ligi Kuu England baina yao na Chelsea siku ya Jumapili.
Kocha huyo mwenye umri wa miaka 54, alionyesha dalili na sasa amelazimika kujitenga mwenyewe ambapo kwa maana hiyo kocha msaidizi wa timu hiyo Pep Lijnders utakaopigwa dimba la Stamford Bridge.
Wachezaji wengine watatu wa Liverpool walibainika kuwa na dalili hizo na watajitenga wenyewe, kupitia taarifa iliyotolewa na klabu hiyo.
Liverpool wanashika nafasi ya tatu kwenye msimamo wa Ligi Kuu England alama moja nyuma ya Chelsea na alama 12 nyuma ya vinara Manchester City.