Kocha Liverpool, Jurgen Klopp amefunguka namna ambavyo alitaka kumsajili Jude Bellingham na mwisho wa siku kujikuta anaangukia kwa Wataru.
Klopp: "Tulimtaka Bellingham lakini tukagundua kuwa haiwezi kutokea".
"Baadae Tulifikiri labda tunaweza kufanya mpango kumchukua Caicedo. Kwahiyo tukafanya taratibu zote ... lakini tukakuta alikuwa na makubaliano ya kihisia tayari na Chelsea pamoja na Pochettino. Kwa upande wa Lavia yeye alikuwa na sababu zake mwenyewe. Kwahiyo tuliishia hapo".
"Hata hivyo bahati iliangukia upande wetu... tumempata Wataru!". Amesema
Je, unadhani usajili wa Wataru ni bora zaidi kuliko Jude Bellingham?