Kocha wa klabu ya Liverpool ya nchini Uingereza Mjerumani Jurgen Klopp amefungiwa mchezo mmoja kutokana na kadi nyekundu aliyopewa mwezi uliopita katika mchezo wa klabu yake dhidi ya Manchester City.
Kwa tafsiri hiyo Klopp atakosekana kwenye mchezo dhidi ya Southampton unaotarajiwa kupigwa katika dimba la AnfieldĀ
Ikumbukwe awali Klopp alipewa faini ya paundi laki tatu 300,000 kama adhabu ya tukio lake la utovu wa nidhamu lakini Chama cha soka nchini humo kilikata rufaa na hatimaye kocha huyo kuongezewa adhabu ya kufungiwa mchezo mmoja wa Ligi Kuu ya EPL.
Katika pambano hilo Liverpool iliibuka na ushindi wa bao 1-0 bao lililofungwa na mshambuliaji wake raia wa Misri Mohamed Salah.