Sat, 18 Dec 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu 15 kati ya 16 zinazoshiriki Ligi Kuu ya Bara zimetoka na azimio la kuunga mkono Udhamini wa Kampuni ya GSM kwenye Ligi hiyo na ziko tayari kuvaa nembo za Mdhamini huyo mwenza wa Ligi hiyo.
Kwa mujibu wa taarifa ya Bodi ya Ligi iliyotolewa vilabu hivyo pia vinepongeza juhudi za TFF na Bodi ya Ligi kusaka wadhamini na zimeomba kuendelea na juhudi za kusaka wadhamini wengine.
Kwa taarifa kutoka vyanzo vya kuaminika zinadai ni klabu moja tu, ambayo ni Simba SC ndio walioshindwa kuafikiana na suala la kuvaa nembo hiyo.
Hii hapa taarifa ya TFF ikifafanua kwa undani;
Chanzo: www.tanzaniaweb.live