Mchambuzi wa soka Bongo, Mkazuzu amasema kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Max Nzengeli kiwango chake kimeshuka.
"Nimekuwa nikimfatilia Max Nzengeli kwenye mechi kadhaa za hivi karibuni hata kama Yanga SC inafanya vizuri either na kushinda lakini Max Nzengeli hafanyi vizuri takriban mechi nne sasa zinafika.
"Confidence yake imeshuka pasi nyingi sio sahihi amekuwa akipoteza mipira hata ule uwezo wake wa kufunga siku hizi ume-drop.
"Anahitaji kujifanyia tathimini na kuona dropping yake inatokana na nini ili mechi zinazofata ule ufanisi na ubora wake urudi kwa sababu anapokuwa kwenye kiwango chake ni moja kati ya wachezaji bora na wenye mchango kwenye kikosi cha Yanga SC."