Sat, 6 Jan 2024
Chanzo: Bbc
Simba imekamilisha usajili wa kiungo mkabaji wa kimataifa kutoka Senegal, Babacar Sarr akiwa mchezaji huru.
Sarr aliwahi kucheza na mastaa wakubwa duniani kama Cristiano Ronaldo wa Al Nassr katika mechi za michuano ya Klabu Bingwa ya Nchi za Kiarabu iliyopigwa Julai 31, mwaka jana wakati akiichezea US Monastir ya Tunisia.
Kiungo huyo mkabaji anayetumia zaidi mguu wa kulia, ametua Msimbazi kuongeza ushindani eneo la ukabaji lenye mastaa kama Mzamiru Yassin, Sadio Kanoute na wengine.
Chanzo: Bbc