Mon, 3 Jul 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa Dodoma Jiji, Christian Zigah ameongeza mkataba wa kuendelea kuitumikia Dodoma Jiji msimu ujao.
Mchezaji huyo alisajiliwa akitokea Biashara United pamoja na Collins Opare na Hassan Mwaterema.
Licha ya kukaa nje kwa muda mrefu kutokana na kuumia msimu uliopita bado ameendelea kuwa chaguo namba moja katika nafasi ya kiungo kwa kocha Melis Medo.
Kiungo huyo alikuwa akicheza na Salmin Hoza, Rajabu Mgalula na Enrick Nkosi katika nafasi ya kiungo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live