Mon, 5 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Yanga imethibitisha kuwa kiungo Salum Abubakari ‘Sure Boy’ atakuwa nje kwa wiki mbili baada ya kupata jeraha la bega kwenye mchezo dhidi ya Kagera sugar.
Akizungumzia hali ya kikosi kuelekea mchezo wa kesho Februari 5, 2024 dhidi ya Dodoma Jiji FC, Meneja wa klabu ya Yanga, Walter Harrison amebainisha kuwa kikosi kipo katika hali nzuri isipokuwa ‘Babu Kaju’ ambaye ameumia bega.
Amesema Sure Boy ambaye kwa mujibu wa Daktari mfupa mmoja wa bega ulihama anatarajiwa kufanyiwa upasuaji mdogo na baada ya wiki mbili atarejea kwenye mazoezi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Related Articles: