Fri, 23 Dec 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa zamani wa PSG, Juventus timu ya Taifa Ufaransa, Blaise Matuidi ametangaza kustaafu soka la kulipwa akiwa na umri wa miaka 35.
“Soka, nilikupenda sana. Soka umenipa mengi, lakini sasa muda umefika wa kusema inatosha. Nimekamilisha ndoto yangu ya utotoni, ndoto yangu ya ukubwani. Najivunia kufunga ukurasa huu leo.” amesema Matuidi.
Matuidi alikuwa sehemu ya kikosi cha Ufaransa kilichobeba Ubingwa wa Kombe la Dunia nchini Urusi 2018.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live