Wed, 27 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ligi ya Ethiopia imekumbwa na Simanzi kufuatia kifo cha Kiungo wa Klabu ya Bahir City ya Ethiopia Alelegn Azene ambaye ripoti zinadai amejiua mwenyewe.
Sababu ya kiungo huyo kujiua bado haijafahamika na hakuwahi kuonyesha dalili zozote za kuwa na changamoto za Afya ya Akili.
Azene alifunga ndoa wiki mbili zilizopita na ndie mchezaji aliekuwa akilipwa mkwanja mrefu Ligi Kuu ya Ethiopia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live