Thu, 29 Feb 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kocha mkuu wa Klabu ya Brighton Hove & Albion Roberto De Zerbi amethibitisha kuwa winga wake Kaoru Mitoma atakuwa nje ya uwanja mpaka mwishoni mwa Msimu kutokana na maumivu ya mgongo.
Mitoma,26, alipata majeraha hayo katika mchezo wa ligi kuu nchini England ambapo Brighton walilazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya Everton wakiwa nyumbani.
" Ni hali mbaya, nadhani tumempoteza Mitoma hadi mwisho wa msimu,".
"Ana jeraha la mgongo, ni tatizo muhimu, atakuwa nje kwa miezi miwili au mitatu."
Chanzo: www.tanzaniaweb.live