Wed, 20 Mar 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo wa klabu ya Tottenham Yves Bissouma (27) amefuta picha zake zote alizokuwa na jezi za timu ya Taifa ya Mali kwenye page zake za mitandao ya kijamii na ku-unfollow page ya shirikisho la soka la Mali (FEMAFOOT) kutokana na kutojumuishwa kwenye kikosi cha Taifa hilo kitakachocheza mechi ya kirafiki dhidi ya Nigeria
Kocha Mkuu wa Mali Sékou Chelle amesema hakumchagua Bissouma kwenye kikosi chake kwa sababu kwa sasa anaona wapo wachezaji wanaomzidi kiungo huyo ambao pia wanafaa kwenye mfumo wake.
Inasemekana Bissouma ambaye pia ana uraia wa Ivory Coast hana maelewano na kocha huyo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live