Mon, 18 Sep 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Zamalek, Emad Abdel-Aziz ameidhinisha kukatwa kwa mishahara ya wachezaji na benchi la ufundi jumla ya dola elfu 5, sawa na zaidi ya shilingi milioni 12 na laki 5 za Tanzania baada ya kipigo cha goli 2 kwa 0 dhidi ya Arta Solar ya Djibout.
Zamalek imeweka rekodi ya kuwa timu ya kwanza ya Misri kufungwa na Timu kutoka Taifa la Djibout. Kabla ya hapo hakuna timu ya Misri iliyowahi kufungwa na timu kutoka Djibout.
Je, kwa bongo ni wachezaji wa timu gani unatamani wakatwe mishahara kutokana na matokeo mabovu?
Chanzo: www.tanzaniaweb.live