Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kisa Wydad Simba wapeleka Mashtaka CAF

Simba Waishtaki WYDAD Kikosi cha Simba SC

Mon, 24 Apr 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Simba SC inatarajia kuwasilisha malalamiko yake kwa Shirikisho la Soka Afrika (CAF) dhidi ya mashabiki wa Wydad AC kuelekea mchezo wao wa marudiano Aprili 28 nchini Morocco.

Miamba hiyo ya Tanzania inachukua hatua hiyo kufuatia tukio lililotokea katika mchezo wao wa kwanza ambapo mashabiki hao maarufu kama Ultras kuruka jukwaa na kuingia VIP B kisha wakawasha fataki zilizopelekea mashabiki na wachezaji kushindwa kuona na hivyo mwamuzi akasimamisha mchezo.

Afisa Habari wa Simba, Ahmed Ally amesema malalamiko hayo yatawasilishwa CAF leo ikiwa ni tahadhari ili mashabiki hao wasiharibu saikolojia ya wachezaji wa Simba.

Simba inakwenda mjini Casablanca ikiwa na mtaji wa goli moja ililopata nyumbani, na hivyo inahitaji kupata sare au ushindi ili kufuzu hatua ya nusu fainali.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live