Makamu wa Rais wa UEFA amejiuzulu kwenye nafasi yake ya kuongoza michezo nchini Sweden baada ya kukosolewa baada ya Shirika la habari za Sky News kuweka wazi kuwa Kiongozi huyo alipiga kura kuitetea Urusi iondolewe marufuku ya kucheza soka Ulaya.
Karl-Erik Nilsson amekiri na kusema kuwa anaelewa imani juu yake haipo tena,hivyo ameamua kuachia ngazi kama mwenyekiti wa Shirikisho la soka la Sweden, takribani miezi minne tangu kushika nafasi hiyo.
Shirikisho la Michezo pamoja na Shirikisho la soka nchini Sweden yalikwishapinga timu za Urusi kuruhusiwa kuwemo kwenye mashindano ya Kimataifa tangu Urusi ilipoivamia Ukraine Februari mwaka jana.