Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kipa Kalambo: Bao la Saido lilikuwa balaa

Bao Saido Pic Data Kipa Kalambo: Bao la Saido lilikuwa balaa

Tue, 22 Dec 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

YANGA imevuna pointi tatu nyingine zilizowafanya wazidi kujikita kileleni, lakini gumzo ni bao tamu la kideoni alililofungwa nyota mpya wa timu hiyo ktoka Burundi, Said Ntibazonkiza ‘Saido’ wakati wakiiangamiza Dodoma Jiji kwa mabao 3-1, huku kipa aliyetunguliwa bao hilo, Aaron Kalambo akishindwa kujiuzuia na kumwagia sifa mfungaji huyo.

Katika mechi hiyo ya Ligi Kuu Bara iliyopigwa Uwanja wa Sheikh Amri Abeid, jijini Arusha Saido akicheza mechi yake ya kwanza ya ligi akiwa na Yanga alifunga bao la pili kwa friikiki na kuasisti jingine la tatu lililowekwa na beki Bakar Mwamnyeto likitokana pia na friikiki yake.

Akizungumza na Mwanaspoti jana juu ya bao hilo la friikiki ambalo lilimfanya aufuate mpira hewani bila mafanikio na kuipa Yanga bao la pili, kipa kalambo alisema mpigaji alikuwa fundi katika pigo hilo, kwani hakutarajia kama angemtungua namna ile.

Kalambo alisema ingawa anajua ana ubora wa kuzuia mipira ya adhabu, lakini kuna sehemu alizembea katika kufungwa bao hilo la pili katika mchezo huo, huku sehemu kubwa akimsifia Saido akidai alitumia akili na ufundi mkubwa kumuadabisha.

Kipa huyo wa zamani wa Taifa Stars, alisema wakati anaupanga ukuta wake katika adhabu hiyo alijua anayetaka kupiga ni mtu bora katika mipira ya adhabu, hivyo alijipa tahadhari akiupanga vyema ukuta wake, lakini akili nyingi za Saido zilimzidi ujanja.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz