Mon, 1 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Winga wa TP mazembe ya Congo DR, Philippe Kinzumbi ameingia kwenye mgogoro na klabu yake hiyo ikiwa ni siku chache baada ya kudaiwa kuwa anatakiwa kuondoka klabuni hapo.
Klabu hiyo inasema bado winga huyo anamkataba nao hadi Juni 2025. Kinzumbi anasema amemaliza mkataba.
Mazembe wanataka walipwe pesa ya usajili na klabu ya Raja Casablanca ama mchezaji huyo aendelee kuitumikia klabu ya Tout Puissant Mazembe.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live