Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kingwendu afurahia sakata la Morrison

Kingwendu+pic Kingwendu afurahia sakata la Morrison

Tue, 11 Aug 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

MSANII wa vichekesho nchini, Rashid Mwinshehe 'Kingwendu' amefurahia filamu inayoendelea kati ya Simba na Yanga, kuhusiana na winga wa kigeni Benard Morrison kwamba yanachangamsha mitandao ya kijamii.

Kinachomchekesha Kingwendu ni povu la mashabiki wanaoonyesheana ubabe, wakiwa hawana uhakika kwamba picha litaishaje, juu ya mchezaji huyo kucheza Simba ama Yanga.

Amesema yeye ni Yanga kindakindaki,jambo lililomfurahisha nikuona timu yake haitaki unyonge nakuamua kupambana, hivyo kama shabiki anapata taswira kuona msimu ujao, taji la Ligi Kuu Tanzania Bara (VPL), litakwenda Jangwani.

"Ujue tulikuwa wanyonge sana kipindi cha ugonjwa wa covid 19, tuliona kama tupo kwenye fumbo fulani hivi, mitandao ya kijamii iliandika vitu vilivyotutia wasiwasi, lakini kwa sasa tumepata vitu vinavyotuchangamsha akili,"

"Ukipita kwenye mitandao ya kijamii, utaona kulivyo kwa moto, wakati Simba inatangaza imemsajili Morrison, mashabiki wa Yanga walitikiswa kama sakata halijamalizika, Simba nayo imetikiswa kwa Senzo Mazingisa yaani ni raha juu ya raha,"amesema.

Amesema Simba na Yanga ziendelee kuwepo ili kuendelea kuwapa raha mashabiki wao, kutokana na vituko vinavyofanywa na klabu hizo.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz