Fri, 10 Jun 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Ndoto za Tanzania Bara kutwaa Kombe la CECAFA Challenge Wanawake 2022 zimeota mbawa baada ya Kilimanjaro Queens kuchapwa 2-1 na Burundi jana Uwanja wa FTC Njeru Jijini Kampala nchini Uganda.
Bao pekee la Kilimanjaro Queens limefungwa na Opa Clement Sanga na sasa Burundi itakutana na Uganda katika Fainali, wakati Tanzania Bara itawania nafasi ya tatu dhidi ya Ethiopia Jumamosi.
Uganda iliichapa Ethiopia 1-0 katika mchezo uliokwenda dakika 120.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live