Staa wa kikosi cha Azam FC, Ibrahim Ajibu amerejea kuna kikosi cha matajiri hao wa Jiji baada ya kukosekana katika michezo kadhaa.
Ajibu ambaye amejiunga na Azam FC katika dirisha dogo akitokea kwa Mabingwa watetezi Simba SC.
Sababu kubwa za kukosekana kwenye kikosi hicho ni matatizo ya kifamilia jambo ambalo limemfanya asiwe kwenye mechi za ligi.
Ajibu alikosekana kwenye mechi tatu ilikuwa miwili ya ligi ilikuwa dhidi ya Ruvu Shooting na Mtibwa Sugar na mchezo mmoja ulikuwa mbele ya Coastal Union huu ulikuwa ni wa Kombe la Shirikisho,
Kwa mujibu wa Ofisa Habari wa Azam FC, Zakaria Thabit amesema kuwa tayari Ajibu amejiunga na kikosi hicho aada ya kumaliza matatizo ya kifamilia.