Tue, 15 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mkutano Mkuu wa 17 wa kawaida wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) umeazimia kuwa kuanzia Januari mwakani mchezaji wa Ligi Kuu hatoruhusiwa kucheza bila kusajiliwa na kulipa ada katika Chama cha Wachezaji (SPUTANZA).
Bosi huyo alisema kwa kila mchezaji anatakiwa kulipa ada ya Sh 120,000 kwa mwaka ambapo kila mwezi ni Sh 10,000.
“Wachezaji wa Ligi Kuu bila kusajiliwa SPUTANZA na kulipa ada hawataruhisiwa kucheza lakini hawa tutafuatilia kupitia klabu zao ambapo ada zitakatwa kwenye mishahara yao, vyama visimamie wanataaluma wake,” alisema Rais Wallace Karia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live