Klabu ya Yanga si mara ya kwanza kufungwa bao tano, je, mlifukuza kocha na maamuzi mengine kama hayo.
Mulifungwa tano na Al Ahly na TP Mazembe mbona hamujafukuza kocha na wala benchi la ufundi?
Kwa maana ranks za Yanga Afrika ndo zinawapa nguvu za kuona hamupaswi kufungwa tano?
Kitu ambacho Simba wanatakiwa kuvumilia na kujua Yanga wapo kwenye form tu nzuri kwa sasa bali hawajaweka Class bado dhidi ya Simba.
Simba wameweka Class yao huu ukanda wa Afrika Mashariki hivyo kufungwa na timu zitakazokuwa kwenye form ni kawaida sana.
English Premier Legue kwa sasa Manchester City ipo kwenye form sana pamoja na hayo bado Manchester United wana Class yao UEFA.
Wamefungwa na wakubwa wenzenu je mungefungwa na timu kama lhefu nafikiri mungetimua mpaka wapishi. Simba wana class yao Afrika wasijishushie heshima yenu pokeeni changamoto.