Kikosi Cha Simba SC kilichosafiri leo saa 10 alfajiri kuelekea nchini Guinea kwaajili ya mchezo wa kwanza wa hatua ya Makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Horoya Athletic Club.
Mchezo huo unatarajiwa kupigwa Jumamosi hii ya February 11, 2023 kwenye Uwanja wa General Lansana Conte nchini Guinea kuanzia saa 19:00 Usiku.
Kikosi hicho kimeondoka na msafara wa watu 45 ambapo wachezaji watakuwa 24 benchi la ufundi pamoja na viongozi wa timu.
Kiungo Mshambuliaji, Saido Ntibazonkiza, Peter Banda pamoja na Jonas Mkude hawatokuwa sehemu ya Wachezaji wanaosafiri kuifuata Horoya Athletic Club kesho na hakuna taarifa yoyote kutoka Simba inayoelezea sababu za Wachezaji hao kutokuwa sehemu ya safari hiyo.
Orodha kamili ya Wachezaji wa Simba SC wanaosafiri kuifuata Horoya Athletic Club ya Guinea kwenye mchezo wa CAF Champions League hatua ya Makundi.
MAKIPA
1:Aishi Manula
2:Beno Kakolanya
3:Ally Salim
MABEKI
4:Shomari Kapombe
5:Gadiel Michael
6:Mohamed Hussein
7:Israel Mwenda
8:Joash Onyango
9:Henock Inonga
10:Mohammed Quatara
11:Kennedy Juma
12:Erasto Nyoni
VIUNGO
13:Sadio Kanoute
14:Mzamiru Yassin
15:Pape Osmane Sakho
16:Kibu Denis
17:Nassor Kapama
18:Ismael Sawadogo
19:Clatous Chama
WASHAMBULIAJI
20:John Bocco
21:Mohammed Mussa
22:Jean Baleke
23:Habibu Kyombo
24:Moses Phiri.