Kikosi cha Wekundu wa Misimbazi, Simba SC na msafara wenye jumla ya watu 45 kinatarajia kuondoka nchini alfajiri ya kesho nchini kuelekea Guinea kwa mchezo wa kwanza wa makundi ya Ligi ya Mabingwa Afrika dhidi ya Horoya ya nchini humo.
Kwa mujibu wa taarifa kutoka Simba APP, msafara huo utakuwa na jumla ya wachezaji 25 wakiwa na benchi la ufundi na viongozi, watasafiri kwa Shirika la Ndege ya Ethiopia kupitia Ethiopia na kubadili ndege mpaka Guienea.
Taarifa hiyo imeeleza, kikosi hicho kinatarajia kufika Guinea kesho jioni na wachezaji kufanya mazoezi ya utimamu wa mwili kuondoa uchovu wa safari.