Kikosi cha Simba kimeanza safari leo Julai 11, 2023 kuelekea nchini Uturuki kwa ajili ya kuweka kambi kujiandaa na msimu mpya ujao 2023/24.
Baada ya ratiba ya mechi za Ngao ya Jamii kutoka, Simba itakuwa na takribani wiki tatu za maandalizi kabla ya kuivaa Singida Fountain Gate FC katika mchezo wa Nusu Fainali ambao utapigwa Agosti 10 katika uwanja wa Mkwakwani Jijini Tanga.
Meneja wa Habari na Mawasiliano klabu ya hiyo, Ahmed Ally amesema kuwa bado hawajamaliza utambulisho, kuna wachezaji wengine wanasubiri kutambulishwa.
“Tunaondoka leo kwenda Uturuki kambini, wachezaji wetu wote watakwenda kushiriki kambi hiyo ya maandalizi. Kocha Robertinho na benchi lake la ufundi wote wako hapa tayari kwa safari”
“Wachezaji wanne wapya tuliowatambulisha nao watajumuika katika kikosi chetu kinachokwenda Uturuki. Bado hatujamaliza, kuna vyuma vingine viwili tutavitambulisha,” amesema Ahmed
Ikiwa Uturuki Simba inatatajiwa kucheza mechi tatu za Kimataifa za kirafiki.
Kikosi Cha Simba kiilichosafiri kwenda nchini Uturuki kwaajili ya pre-season ni;
MAKIPA
Ally Salim
Ahmed Feruzi
MABEKI
Shomari Kapombe
Mohamed Hussein
Henock Inonga
David Kameta
Israel Mwenda
Kennedy Juma
Jimson Mwanuke
Che Fondoh Malone Junior
VIUNGO
Claoutas Chma
Sadio Kanoute
Mzamiru Yassin
Nassoro Kapama
Aubin Kramo Kouamé
Saido Ntibanzonkinza
Peter Banda
Pape Osmane Sakho
WASHAMBULIAJI
Willy Essomba Onana
Baleke Othos Baleke
John Raphael Bocco
Moses Phiri
Kibu Denis
Mohamed Mussa