Thu, 30 Mar 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kikosi kamili cha Arsenal kimerejea katika viwanja vya mazoezi vya London Colney kwa ajili ya maandalizi ya mechi ijayo ya EPL dhidi ya Leeds Utd Jumamosi hii Aprili 1.
Kiungo wao Thomas Partey amefanya mazoezi na Wachezaji wenzake licha ya kushindwa kucheza mechi ya AFCON dhidi ya Angola akiwa na Taifa lake la Ghana wakidai kuwa alipata majeraha madogo lakini ana matumaini ya kuwa fiti kumenyana na Leeds.
Hadi sasa Haijulikani kama beki wao William Saliba atacheza dhidi ya Leeds. The Gunners watatathimini hali ya uponaji wa jeraha lake kabla ya kumruhusu kurejea dimbani.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live