Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kigogo Simba SC atua Mamelodi Sundowns

CEO Simba Atua Mamelodi CEO wa Simba SC, Imani Kajula akiwa na Viongozi wa Klabu ya Mamelodi

Thu, 16 Mar 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Katika kuendeleza mahusiano yenye tija baina yake na klabu kubwa barani Afrika, wiki hii, Afisa Mtendaji Mkuu wa klabu ya Simba SC, Imani Kajula, ametembelea miamba ya soka Afrika kwa sasa, Mamelodi Sundowns.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka Simba, lengo la ziara hiyo ni kujenga mahusiano mazuri na taasisi pamoja na klabu za mpira ili kukuza ushirikiano na kubadilishana uzoefu katika mambo mbalimbali ya maendeleo.

Akiwa makano makuu ya miamba hiyo nchini Afrika Kusini, CEO Kajuna amekutana na Mwenyekiti wa Sundowns, Tihopie Motsepe, Mkurugenzi wa Ufundi Flemming Berg na Mkuu wa Mashindano Stanley Mabulu.

Viongozi hao wamejadiliana mambo mbalimbali ya kimaendeleo ya soka, miundombinu yake na jinsi ya kujikwamua kutoka Simba ilipo hadi kufika ngazi za juu ambazo wanatamani kufika.

Mwezi uliopita, Simba iliwaalika Al Hilal ya Sudan na kuwawezesha kupata kambi ya wiki mbili kujiandaa na michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika ikiwa ni sehemu ya ushirikiano kati yao na miamba hiyo ya Sudan.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live