Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kifaru awakumbusha Yanga kipigo cha Ihefu

Manungu Turiani Morogoro Kifaru awakumbusha Yanga kipigo cha Ihefu

Sat, 31 Dec 2022 Chanzo: Mwanaspoti

Leo Jumamosi, Mtibwa Sugar ni mwenyeji wa Yanga katika mchezo wa mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara utakaochezwa kwenye Uwanja wa Manungu huku wakiahidi ushindi.

Thobias Kifaru ambaye ni Msemaji wa Mtibwa Sugar amesema kuwa pamoja na kwamba Yanga ni mabingwa watetezi na wanapambana kuhakikisha wanatetea ubingwa wao lakini wao wamejipanga kuwa timu ya kwanza kuharibu mipango ya wapinzani wao.

Kifaru ameendelea kutamba kuwa wana kikosi bora japokuwa mzunguko wa kwanza walikubali kipigo cha mabao 3-0 lakini hiyo sio sababu kwao ya kuendelea kufungwa na Yanga.

"Tunakutana wote ni bora, hivyo kutakuwa na kazi ngumu kweli kweli ndani ya dakika 90, Yanga ilifungwa na Ihefu mzunguko wa kwanza, sisi tunawaharibia mzunguko wa pili na hawataamini," amesema Kifaru

Msemaji huyo ameendelea kuweka wazi kuwa hawana hofu yoyote na mchezo huo na ndio maana wamewapokea wazee wa Yanga na kuwaacha kufanha mambo gao watakavyo uwanjani.

"Jioni ya jana Yanga walitakiwa waje kufanya mazoezi hapa lakini amekuja kiongozi wao Saleh Hafidh kukagua uwanja nimempokea na akaondoka, baadaye wakaje wazee wao nao nimewapokea na kuwaacha huru kwa saa kama mbili uwanjani walikuwa wanafanya yao nao wakaondoka.

"Mpira sio uadui ndio maana tumewapokea vizuri na hatuna hofu yoyote na fitina, tumewaacha wafurahi kama mashabiki watakavyofurahi kesho wakati wa mechi na muda ndio utaamua na si vinginevyo."

Aidha, Kifaru amezungumzia bahati waliyoipata Yanga msimu uliopita na msimu huu kuwa; "Hali ya hewa inawajia vizuri Yanga huku kwetu hakuna mvua tofauti na Simba wana bahati mbaya walikuja kipindi cha mvua kubwa hatukuonyesha soka safi."

Timu hizo zote zinakutana zikiwa zimecheza mechi 18, Yanga ipo kileleni na pointi 47 wakati Mtibwa Sugar wakishika nafasi ya nane kwa pointi 24.

Chanzo: Mwanaspoti