Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kifaa kipya Yanga hiki hapa

Jembe Pic 1 Data Kifaa kipya Yanga hiki hapa

Wed, 16 Dec 2020 Chanzo: mwanaspoti.co.tz

YANGA inapambana kupata saini ya straika namba moja wa DC Motema Pembe ya DR Congo, Dark Kabangu, Mwanaspoti linajua.

Kama Yanga itafanikiwa kumnasa mchezaji huyo utakuwa usajili wa pili wa Kocha Cedrick Kaze baada ya ule wa Saido Ntibazonkiza wa Burundi ambaye kuanzia leo atakuwa huru kuichezea Yanga. Dirisha dogo la usajili limefunguka usiku wa kuamkia leo huku Saido akiwa mchezaji huru.

Habari za uhakika ambazo Mwanaspoti imezipata jana kutoka DRC ni kwamba wakala wa Kabangu ndiye anayewasimamia pia Mukoko Tonombe na Tuisila Kisinda na mazungumzo yanaendelea baina ya vigogo wa Yanga ila ugumu upo mmoja tu. Kabangu anataka Yanga imvumilie mpaka baadae mwezi Januari akacheze michuano ya CHAN nchini Cameroon jambo ambalo limeibua sintofahamu. Kabangu amewahi kucheza soka Hungary na Armenia na Yanga walikuwa wakimuwinda tangu mwaka jana ila wakashindwana dau.

Habari zinasema kwamba Yanga wanaendelea kumshawishi straika huyo mzoefu lakini ikishindikana kabisa wiki hii watafanya uamuzi mwingine. Vyombo vya habari vya Kinshasa vimeripoti kwamba Yanga wana uwezekano mkubwa wa kumpata Kabangu mwenye mabao sita msimu huu ingawa Mwanaspoti linajua bado kikwazo ni michuano hiyo ambayo anataka kwenda kucheza aweke rekodi na kuongeza soko lake.

Kaze ameiambia Mwanaspoti wiki hii kwamba; “Nataka straika mmoja wa maana sana, lakini bado napitia rekodi za wachezaji mbalimbali nilionao ndio nifanye uamuzi.” Kocha huyo ambaye ametimiza siku 55 ndani ya Yanga aligoma kuweka wazi majina aliyonayo ingawa mashabiki wameonekana kukubali mafanikio yake na kuwa na shauku ya kujua anayemshusha tena atakuwaje.

Chanzo: mwanaspoti.co.tz