Kiungo wa zamani wa Timu ya Taifa ya Tanzania Taifa Stars , Simba, Yanga na Azam FC Amri Kiemba amewasifu viungo mahiri wa Simba na Yanga, Clatous Chama na Khalid Aucho.
Kiemba amekwenda mbali na kusifu namna viungo hao wanavyoleta uhai katika timu zao huku akieleza kuwa katika kipindi cha uchezaji wake kama angepata nafasi ya kucheza na mmoja wa viungo hao basi hakika angekuwa mbali sana katika Career yake ya soka.
Akizungumza Kiemba anasema;
“Nimecheza na viungo wengi katika nchi yetu, lakini katika hawa viungo wa sasa ningetamani kucheza na Timu moja na Khalid Aucho na Clatous Chama, nahisi ningekuwa bora maradufu"