Thu, 18 Jan 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Klabu ya soka ya Singida Fountain Gate, Japhet Makau kupitia Bodi ya Wakurugenzi amemteua Bi Kidawawa Tabitha kuwa Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) mpya wa klabu hiyo.
Ms Kidawawa kabla ya uteuzi huo alikuwa akitumikia nafasi ya Mkurugenzi wa Masoko na Biashara ndani ya Klabu hiyo.
Uteuzi huo ni sehemu ya mabadiliko ya kimkakati yanayoendelea ndani ya klabu hiyo yenye maskani yake mkoani Singida ili kuongeza ufanisi na weledi.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live