Mchambuzi Shafii Dauda amewatetea wachezaji wa Simba SC kwa kufungwa na Yanga SC goli 5-1.
Shafii amesema viongozi wanapaswa pia kulaumiwa.
“Simba wamekosa kutengeneza succession plan , mfano leo nimesikia watu wanawakosoa Kapombe , Zimbwe na Chama , hawa wachezaji wameshinda kila kitu kwa misimu minne unataka wakupe nini ?”
“Kuna wachezaji wana zaidi ya miaka 10 wanacheza , sio sawa kulaumu wachezaji unapaswa kuwalaumu viongozi na mfumo wao kwa kushindwa kutengeneza wachezaji wengine kuja kuwasaidia majukumu hawa wengine “
“Hawa wanaowashutumu kina Zimbwe na Kapombe hawawatendei haki ndio waliopo”