Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kibu anaufanya mpira uonekane mchezo mgumu

Kibu D KIBU DENGA.jpeg Kibu anaufanya mpira uonekane mchezo mgumu

Mon, 22 Apr 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Playing football is very simple, but playing simple football is the hardest thing there is.Johan Cruyff

Johan Cruyff aliamini sana kwenye nadharia yake ya kucheza mpira ni rahisi sana lakini kucheza mpira rahisi ni kitu kigumu kwasababu

1.Alitaka kuona wachezaji ambao wanafanya vitu rahisi kuurahisisha mchezo bila kutumia nguvu nyingi hasa kipindi wana mpira.

2.Alitaka kuona ubongo unafanya kazi kuliko fuvu la kichwa yaani akili kwanza akili mwisho.

Uenda kaburi la Johan Cruyff likawa linatingisha kwasababu ya kile anachokifanya Kibu Dennis akiwa na mpira mguuni kwasababu kuna muda Kibu anafanya vitu ambavyo havina maana

1.Kibu akiwa na mpira anataka kukimbia nao Kila muda kitu ambacho kinawafanya wapinzani kuendelea kujiimarisha kwenye muundo wao kuzuia.

2.Kibu ubongo wake kuna muda unashindwa kujua kwamba mpira unatakiwa kutembea kuliko yeye kipindi timu ina mpira (in possession).

3.Kibu kuna muda anashindwa kutafuta nafasi kwenye maeneo muhimu kwa ajili ya kupasia mpira kirahisi kabisa.

Kibu Denis mchezaji wa kisasa kabisa lakini changamoto kubwa hafahamu muda wa kukimbia na mpira na muda wa kupamiana na wachezaji wa timu mpinzani,kukimbia sana na mpira katika tafsiri ya soka la kisasa ni kuvifanya vitu vizuri kwa njia ngumu.

Binafsi nafikiri wachambuzi wala rushwa na mashabiki wavivu wa kufikiri sahihi kuna sehemu wanashindwa kumsafisha Kibu Denis matongotongo vizuri wanampa sifa za kijinga eti anakaba sana na kuwasumbua mabeki wameshindwa kabisa kumwambia Kibu kuna upande wa shillingi wa kucheza mpira rahisi kabisa kwenye njia rahisi.

Nendeni kwenye kaburi la Johan Cruyff mkachukue ubongo wake kisha muuweke kwenye kichwa Cha Kibu.

If truth shall kill them let them die.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live