Kocha Mkuu wa Tabora United, Goran Kopunovic leo Ijumaa asubuhi, Septemba 15, 2023 amezungumza na waadishi wa habari kuelekea mechi yao ya Ligi Kuu ya NBC dhidi ya Tanzania Prison.
"Tunatambua utakua mchezo mgumu sana kesho dhidi ya Tanzania Prison lakini tumejiandaa vizuri. Huu ni mchezo wetu wa kwanza kucheza nyumbani katika msimuu huu na mchezo wa kwanza baada ya miaka tisa kupita timu ya Tabora kucheza katika uwanja huu.
"Tunahitaji kuweka historia nzuri baada ya mda mrefu kupita kwahiyo tunahitaji kupata ushindi. Mashabiki waje kwa wingi kutupa sapoti tuandike historia hii nzuri kwa pamoja," amesema Kocha Goran Kopunovic.