Kocha wa timu ya taifa ya Kenya (Harambee Stars) Engin Firat akielezea kuhusu uwezekano wa Kenya kufuzu Kombe la Dunia la 2026 nchini Marekani, Mexico, Canada.
"Kila timu Inaonekana Ina uwezo wa kushinda Dhidi ya yeyote, Hii itatengeneza faida kwetu. Nina matumaini makubwa kuhusu siku zijazo. Nadhani tuna uwezekano mkubwa wa kwenda Kombe la Dunia."
Katika Kampeni za Kutafuta Nafasi ya Kufuzu kombe la Dunia 2026, Kenya iko kundi F pamoja na Ushelisheli, Gambia, Ivory Coast, Burundi na Gabon. Atakaye Ongoza Kundi Atafuzu Moja kwa Moja Kushiriki Kombe la Dunia.
Unaiona Kenya ikishiriki Kombe la Dunia 2026? Tupe utabiri wako