Fri, 12 Jul 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Klabu ya Simba imethibitisha kuinasa saini ya mlinzi wa kulia, Kelvin Kijili kutoka Klabu ya Singida Fountain Gates kwa mkataba wa miaka 2.
Kijili (24) aliisaidia Singida Fountain Gates (Fountain Gates) kumaliza nafasi ya 11 kwenye ligi msimu 2023/2024 kwa kutoa pasi za magoli (assists) 4 msimu uliopita.
Kijili anatajwa kuwa ndiye mbadala sahihi wa Shomari Kapombe, ni mchezaji mwenye kipaji na kasi amekuwa akitumika kuanzisha mashambulizi kutokea upande wa kulia.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live