Thu, 24 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Kiungo Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Ubelgiji, Kelvin De Bruyne ameshangaa baada ya kupewa tuzo ya mchezaji Bora wa mechi (Man of the Match) wakati timu yake ilipopanda dimbani jana kucheza na Canada.
Katika mchezo huo wa Kundi F wa Kombe la Dunia, Ubelgiji ilishinda kwa bao 1-0, bao ambalo lilifungwa na Michy Batshuayi dakika ya 44.
"Sifikirii kama nilicheza Kwa Kiwango kikubwa sana. Sijui kwanini nimepewa Tuzo hii (Tuzo ya Mchezaji Bora wa Mechi).Labda ni Kwa sababu ya jina langu," amesema De Bruyne.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live