Fri, 24 Sep 2021
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Uongozi wa klabu ya Young Africans SC, umemtambulisha Cedric Kaze kama kocha msaidizi wa kikosi hicho.
Kaze anakwenda kushirikiana na Kocha Mkuu Nasreddine Nabi katika kuhakikisha timu hiyo inafanya vyema msimu ujao.
Wakati huo huo Yanga wamemtambulisha Mwinyi Zahera kuwa Mkurugenzi wa Maendeleo Soka la Vijana.
Zahera na Kaze wote kwa nyakati tofauti wamepata kuhudumu ndani ya Klabu ya Yanga kama Makocha wakuu.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live