Wed, 9 Nov 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Wenyeji, Singida Big Stars wamekwenda sare ya kufungana bao 1-1 na Simba SC katika mchezo wa Ligi Kuu ya Tanzania Bara jioni ya leo Uwanja wa LITI mjini Singida.
Kiungo mshambuliaji, Deus Kaseke alianza kuifungia bao Singida Big Stars dakika ya 11, kabla ya winga Mmalawi, Peter Banda kuisawazishia Simba SC dakika ya 79.
Kwa sare timu zote zimafikisha pointi 18, Simba ikibaki nafasi ya pili katika mchezo wa tisa na Singida nafasi ya nne katika mchezo 10.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live