Mon, 17 Oct 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Mshambuliaji wa Real Madrid na Timu ya Taifa ya Ufaransa, Karim Benzema amenyakua tuzo ya Ballon D'or 2022 baada ya kuwa na msimu bora kabisa 2021/2022.
Benzema amenyakua tuzo hiyo akiwabwaga Sadio Mane (Bayern Munich) aliekamata nafasi ya pili na Kevin de Bruyne(Man City) aliekamata nafasi ya tatu.
Msimu wa 2021/2022, Benzema amebeba La Liga na Ligi ya Mabingwa barani Ulaya akiwa na Real Madrid wakiichapa Liverpool.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live