RAIS wa shirikisho la soka Tanzania (TFF), Wallace Karia amekabidhiwa jezi za Simba na Yanga kwa ajili ya kutinga nazo katika dimba la Benjamin Mkapa wakati wa michezo ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo vilabu vya Simba na Yanga vitapeperusha bendera ya Tanzania.
RAIS wa shirikisho la soka Tanzania (TFF), Wallace Karia amekabidhiwa jezi za Simba na Yanga kwa ajili ya kutinga nazo katika dimba la Benjamin Mkapa wakati wa michezo ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika ambapo vilabu vya Simba na Yanga vitapeperusha bendera ya Tanzania. Simba Sc itashuka dimbani Benjamin Mkapa kukabiliana na Al Ahly ya Misri siku ya Ijumaa Machi 29, 2024 huku Yanga Sc ikiikaribisha Mamelodi Sundowns siku ya Jumamosi Machi 30, 2024.