Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kapombe: Mechi ngumu, tumejipanga

Kapombe Pic Data Simba wataikaribisha Asec Mimosas kwa Mkapa

Tue, 8 Feb 2022 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

Beki wa Simba, Shomari Kapombe amesema wanatambua ugumu wa mechi ya Jumapili dhidi ya Asec Mimosas, mchezo wa kwanza wa hatua ya makundi ya Kombe la Shirikisho Afrika (CAF).

Kapombe amesema wanajiandaa vilivyo kuhakikisha wanapata ushindi mnono, utakaowapa nguvu katika mechi ya ugenini.

"Tunajua utakuwa mchezo mgumu, lakini tumejipanga kuhakikisha mashabiki wetu wanaondoka na kicheko kitakachotokana na ushindani tutakaotoa" amesema Kapombe na kuongeza;

"Tunahitaji kusonga mbele zaidi, kwani Simba ndio timu pekee inayoliwakilisha taifa kimataifa."

Simba imefanya mazoezi leo Februari 8 jioni katika uwanja wa Mo Simba Arena, uliopo  Bunju jijini Dar es Salaam.

Hata hivyo sio kikosi kizima kilichomfanya  mazoezi leo, kutokana program aliyoiweka kocha wa timu hiyo, Pablo Franco.

Wachezaji ambao wamefanya mazoezi katika uwanja huo ni wale walioingia katika mchezo uliopita wa ligi dhidi ya Mbeya Kwanza na ambao hawakucheza kabisa.

Mastaa hao ni Beno Kakolanya, Ally Shomari, Pascal Wawa,Erasto Nyoni, Kennedy Juma, Joash Onyango, Mzamiru Yassin, Israel Mwenda, Gadiel Michael, Peter Banda, Clatous Chama na Hassan Dilunga ambaye ameumia na kutolewa nje.

Mastaa ambao hawakuwepo, walipangiwa programu ya gym.

Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz